Sunday, January 15, 2017

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE...AMANI NA FURAHA ZITAWALA KATIKA NYUMBA ZETU!

Zipo furaha nyingi duniani, watu wanafurahia kufaulu mitihani, kupata ajira, mtoto, kuoa na kuolewa, kuwa na mali nyingi na mambo mengi kadha wa kadha. Lakini hebu tuone furaha iliyo kuu kuliko zote, "Ndipo wale sabini  waliporudi kwa furaha wakisema hata pepo wanatutii, YESU akawambia msifurahi kwa vile pepo wanawatii BALI FURAHINI KWA SABABU MAJINA YENU YAMEANDIKWA MBINGUNI. Kumbe furaha kuu ni jina lako kuwa limeandikwa katika kitabu cha uzima. Luka 10:17-20".  JUMAPILI NJEMA.

No comments: