Thursday, October 13, 2016

JIPE MOYO KAMWE USIKATE TAMAA KWA MUNGU YOTE YANAWEZEKANA

"Nilikuwa naangalia mpira wa miguu katika uwanja wa shule. Nilipokaa, nilimuuliza kijana mmoja juu ya matokeo ya mchezo. Kwa tabasamu, alijibu "Wako mbele yetu 3-0"! Nikasema, Kweli!! Mbona huonekani kukata tamaa.
"Kukata tamaa? "Yule mvulana aliuliza kwa mshangao.... Kwanini nikate tamaa wakati bado refa hajapuliza kipenga cha mwisho? Nina imani na timu yangu na meneja wa timu; Nina hakika tutashinda! Na kweli, mchezo uliisha 5-4 timu ya kijana ikiwa mbele! Alinipungia mkono taratibu, na tabasamu zuri akiondoka uwanjani; nilishangaa,mdomo wazi, ujasiri mkuu kiasi hiki; nilipenda alivyojiamini ;  Nilipofika nyumbani usiku ule, swali lake lilizidi kuja kwangu zaidi.
"Kwanini niogope wakati refa hajapuliza kipenga cha mwisho?" Maisha ni kama mchezo. Kwanini ukate tamaa wakati Mwenyezi Mungu ndiye meneja wako? Kwanini ukate tamaa wakati kungalipo uhai ndani yako? Kwanini ukate tamaa wakati kipenga chako cha mwisho bado hakijapigwa? Ukweli ni kwamba watu wengi hujipulizia wenyewe vipenga vyao vya mwisho. Lakini madamu ungalipo uhai, hakuna kisichowezekana muda haujakuacha. 
Nusu kipindi si kipindi kizima na ratiba ya Mungu kwa mwanadamu si ratiba ya mwanadamu kwa Mungu.
Usijipulizie kipenga chako cha mwisho wewe mwenyewe.
UJUMBE- Maisha ni changamoto  ambapo pia ni kama mchezo...twapaswa kuwa jasiri na kujiamini.

No comments: