Monday, April 11, 2016

JUMATATU HII TUANZE HIVI! UNYWAJI WA TANGAWIZI NA FAIDA ZAKE KUMI UTAKAZOPATA UKIANZA KUNYWA LEO...!!

1. Huondoa halafu mbaya ya kinywa:-
Tofauti na vyakula vingine kama kitunguu swaumu. Tangawizi husaidia uwe na halafu nzuri pale unapopumua na kufanya maeneo ya mdomo kuwa safi.
2. Msukumo wa damu:-
Tangawizi husaidia msukumo wa damu mwilini kwa sababu huupa mwili joto ambalo mara nyingi mwili huhitaji wakati wa usukumaji wa damu mwilini
3. Huondoa magonjwa ya asubuhi:-
Licha ya kuwa tiba ya magonjwa kama kikohozi na mafua, tangawizi pia husaidia kupunguza magonjwa ya asubuhi kama uchovu na mninginio. Kwa akina mama wajawazito, tangawizi huwapunguzia homa za asubuhi wanapoamka, pia hutumika kama kichocheo cha utulivu.
4. Mfumo wa chakula:-
Husaidia mwili kunyonya virutubisho kwenye chakula. Hii husaidia sana pale unapoamua kupunguza uzito wa mwili na kupata virutubisho vilivyo muhimu.
5. Kurekebisha sukari ya mwili:-
Tangawizi husaidia katika kuweka sawa kiwango cha sukari kwenye damu. Wagonjwa wa kisukari wanashauriwa kutumia tangawizi badala ya chai.
6. Hamu ya kula:-
Huongeza hamu ya kula chakula. Kwa wale wenye mfumo mbaya wa umengényaji wa chakula wanashauriwa kutumia tangawizi ili kupata mfumo mzuri wa mmengényo wa chakula.
7. Uzalishaji wa mate:-
Tangawizi  husaidia uzalishaji wa mate mdomoni. Kuongezeka kwa mate mdomoni husaidia kutengeneza vichocheo muhimu vinavyosaidia wakati wa kula na kupunguza  uwezekano wa magonjwa ya meno.
8. Kuyeyusha mafuta
Tangawizi husaidia kupunguza kuganda kwa mafuta mwilini ambayo yana madhara makubwa mwilini. Hasa magonjwa ya kiharusi na shinikizo la damu.
9. Kuondoa sumu mwilini:-
Tangawizi husaidia kupunguza kichefuchefu na kutapika. Pia husaidia sana kwa wale watu waliotumia sana madawa na kuwa na sumu nyingi mwilini.
10. Tangawizi humsaidia mtu mwenye vidonda vya tumbo kwa kupunguza maumivu na hata kuponya vidonda hivyo kama vitakuwa kwenye hatua ya awali sana.
PANAPO MAJALIWA!!!

No comments: