Sunday, January 31, 2016

JANA JUMAMOSI YA TAREHE 30 /1/2016 ILIKUWA KUMBUKUMBU YA MT.YASINTA MTAWA...

Mt Yasinta Mtawa

Leo tunamkumbuka Mt Yasinta mtawa.Alizaliwa Viterbo,Italia mwaka 1585.Alisoma katika shule ya masista hapo Viterbo.Yeye alilazimika kuingia utawa katika shirika la  Wafranciscan,baada ya kuugua na kuitiwa Padri kwa ajiri ya kumkomunisha.Padri alipoingia chumbani kwake,aliona kuwa  Mt Yasinta aliishi maisha mabaya.Padri alimshauri kubadili mfumo wa maisha yake.Aliingia utawa,akafuata ushauri wa Padri.Miaka 24 baadaye,akiwa mtawa,aligeuka kuwa mfano wa kila kitu chema.Tabia njema,UchaMungu,na kusaidia watu wote.Alikufa mwaka 1640 Januari 30.Alitangazwa mwenyeheri  Septemba 1,1726.Alitangazwa mtakatifu mwaka 1807 Mei 24 na Papa Pius wa Vll

Watakatifu wengine wa Leo ni

Mt. Aldegunais
Mt. Aleaunie
Mt. Alexander
Mt. Armentarius
Mt. Armentarius
Mt. Barsimaeus
Mt. Bathildis
Mt. Felician
Mt. Hippolytus
Mt. Martina of Rome
Mt. Matthias wa Jerusalem
Mt. Mutien-Marie Wiaux
Mt. Savina wa Milan
Mt. Tudy
NAWATAKIENI WOTE JUMAPILI  NJEMA! NA TUMWOMBE MT. YASINTA  ATUOMBEE WOTE!

No comments: