Thursday, April 16, 2015

MWANAMKE KANGA....NIMEPENDA MTINDO HUU WA KUFUNGA KANGA!!

Kanga zina matumizi mengi sana. Ni utamaduni mzuri sana ..ila naona kama unaanza kupotea. Nikisema hivi nina maana wanawake wengi wameanza kuacha kutumia kanga na kuiga mavazi mengine kabisa inasikitisha kwa kweli maana kiazazi kijacho hakitajua utamaduni huu. Tafadhali wanawake wenzangu tudumishe utamaduni huu. Kapulya.

4 comments:

Rachel Siwa said...

kapendeza mwayego..!!
Ni kweli Kadala wa mimi..
sasa niwakati mimi wewe na yule tuanze kuvaa kanga na kuweka picha kwa mitandao tulivyopendeza na vazi hilo..
Lakini sina uhakika kama ninazo za kutoshaaa......mwehh.

Anonymous said...

Mambo ya khanga

Yasinta Ngonyani said...

Kachiki kama huna za kutosha sema maana mimi nanizo halafu dada Mariamu wa Japan atatuunga mkono nadhani.

Candc! Ndiyo mambo ya Kanga kwani vipi hupendi?

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Ulimbukeni na kupwakia vya wengine kunaua mambo mengi. Mara jeans mara ninja mara upuuzi mara kila cha wenzao cha maana. Huoni hata akina kaka wanavyovaa milegezo na kutoboa masikio utadhani kuna biashara wanatangaza wasijue chanzo na maana ya yote.