Tuesday, October 28, 2014

KUMBUKUMBU:- KWANZA NIMETAMANI UGALI WA MUHOGO!!!!

Hii kazi hii ilikuwa kazi ya karibu kila siku maana usipotwanga mihogo hakuna ugali...basi hapo unapomaliza kutwanga uso mzima ni kama vile umemwagiwa unga...Tulikuwa tukipaka usoni kama poda mweeeeee...kaaaazi kwelikweli. Nimekumbuka sana enzi zila na pia nimetamani ugali wa muhogo na kisamvu chake...si unajua hakitupwi kitu maganda ni chakula cha nguruwe  mmea mzuri sana huu

6 comments:

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Da Yacinta nakubaliana nawe: Ya kale dhahabu japo ukifanya hivyo unaonekana mshamba na anayeturudisha nyuma. Afrika hakuna ma-junk ati. Huo ugali wa muhogo au bada usiambiwe.

Rachel Siwa said...

Raha ya nyumbani,chakula bora,hakuna upweke...
Asante Sana Kadala.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Mhango ..lakini wakati mwingine ni afadhali kuonekana mshamba huku ukijali utamaduni wako
KACHIKI! chakula kama hiki ni bara sana ila inasikitisha wengi wameaacha kula ...

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Da Yasinta nakubaliana nawe. Huwa sisikilizi anachosema mtu bali unachosema moyo wangu. Ushamba wangu hahumhusu yeyote. Usijali kuonekana mshamba. Maana kuna kipindi anayeweza kukuona wewe mshamba akawa mshamba kuliko wewe na anayekuona mbaya akawa mbaya kuliko wewe. Hivi mtakatifu Kitururu mna mawasiliano? Nilipita ugani kwake nikakuta ametekwa kama ulivyokuwa umefanyiwa.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Mhango nimekupata...Mtakatifu nimeona hapa kwake haiwezekani kuingia nitampa taarifa

obat cytotec said...

obat telat bulan i think your blog very informative cytotec thanks for sharing obat penggugur