Friday, December 14, 2012

BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIA KUTOKUWA HEWANI KWA MUDA ..NAKWENDA KULA LIKOLO LA NANYUNGU:-)NYUMBANII NI NYUMBANI!!!

Hali ya hewa ndivyo ilivyo leo  DAKIKI/DAKIKA MBILI ZILIZOPITA...yaani mtu unaonekana mnene kama vile tembo kwa ajili ya kuvaa mingua mingi ili usisikie baridi. Nina furaha kuachana na hali hii kwa muda .. nisemapo hivi ni kwamba BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIA INATAKA KUSEMA HAITAKUWA HEWANI KWA MUDA KUTOKANA NA MAMA WA MAISHA NA MAFANIKIO ATAKUWA SAFARINI. Nachukua nafasi hii kuwatakieni wote CHRTITMAS NJEMA NA PIA MWAKA MPYA NA PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA HAPO MWAKANI 2013.
Labda tu Remmy Ongala afichue wapi nakwenda..... na kipande hiki cha mziki..

Narudi nyumbani eeeeh nakwenda kula likolo la nanyungu....wangoni wote myumwike..nyumbaniiiiiii

Wednesday, December 12, 2012

NIMEUPENDA UBUNIFU HII ...AKILI NI MALI KILA MTU ANA ZAKE/USITUPE VIZIBO VYA BIA/SODA NI MALI!!!

Mwaka jana nilipita Mikumi katika maduka waozayo mambo ya urembo na vitu vingine..Nilishikwa na mshangaO baada ya kuona hizi heleni zilizotengenezwa na vizibo vya sodana bia (visoda). Nilipenda sana ubonifu wao na binti yangu akaniambia twaweza pia kufanya kazi hiyo kwa mikono yetu. Lakini, kumbe si kazi rahisi. Nawasifu watu waliofanya kazi hii kwa mikono yao. kunywa soda au bia yako na vizibi ( visoda ) usitupe ni mali... NAWATAKIENI WOTE SIKU HII YA JUMATANO IWE NJEMA SANA NI SIKU MAALUMU MAANA NI TAREHE 12-12-12..KILA LA KHERI!!!

Tuesday, December 11, 2012

KUMBUKUMBU .....TANZANIA!!!!!

 Shamba la katani ...ni Morogoro karibu na mlima wa Uluguru


Twiga wa Serengeti
Ngorongoro Crater

Sunday, December 9, 2012

JUMAPILI YA LEO NI JUMAPILI AMBAYO IMEANGUKIA SIKU AMBAYO TULIPATA UHURU 9/12/1961...


Nami nimea si wimbo huu wa maombi unafaa sana kwa siku ya leo. NACHUKUA NAFASI HII NA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA NA PIA SIKU HII KWA UJUMLA

Friday, December 7, 2012

SALAMU/UJUMBE KUTOKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IJUMAA YA LEO NI:-

Kila CHOZI ni ishara ya MAUMIVU. Kila ukimya ni ishara ya UPWEKE, kila TABASAMU ni ishara ya FURAHA, lakini kila ujumbe ni ishara ya kum-mis/kumtamani mtu. NAWATAKIENI WOTE MTAOPITA HAPA  ASUBUHI ,MCHANA, JIONI AU NISEME TU IJUMAA NJEMA.....KAPULYA!!!!

TUANZE MWISHO WA JUMA HILI NA WIMBO HUU MALAIKA NAKUPENDA NA MIRIAM MAKEBA....


NAPENDA KUWATAKIENI WOTE MWISHO MWEMA WA JUMA NA MATUMAINI YANGU TUPO PAMOJA...KAMA UTAKUWA UNAENDESHA WALE WENYE THERUJI ENDESHENI TARATIBU MAANA KUNA AJILI NYINGI ZIMETOKEA MPAKA SASA..IJUMAA NJEMA....

Nilipoendelea kutafuta zaidi wimbo huu wa MALAIKA...nikakutana na hawa nadhani ni wachina nao wanaimba ebu wasikilize ukipata muda....

Kweli kiswahili sasa kinaenea dunia nzima....haya kila la kheri!!!!

Thursday, December 6, 2012

JINSI WATOTO WA KIKE WANAVYOJIFUNZA MAISHA ...

....mtoto umleavyo ndivyo akuavyo..ila kuna wakati katika jamii yetu huwa tunazidisha kidogo..mtoto anakuwa kama mtu mzima kabisa. Kwa maana hiyo anakosa ule muda wa kuwa mtoto. Ila tumejifunza mengi na tumekuwa kwa kiutu uzimauzima si kama sasa..au wenzangu mliopitia maisha haya mnasemaje?..Duh!  siku zinakimbia tayari leo ni Alhamisi ya tarehe 6/12/2012..KILA LA KHERI WANDUGU!!!!

Wednesday, December 5, 2012

MCHANA WA LEO NINGEPATA MLO KAMA HUU NINGEFURAHI SANA LAKINI SASA ITANIBIDI NILE KWA MACHO....

Ni ugali kwa mlenda uliochanganywa kwawa majani ya maboga na ambayo bamia. Halafu  bakuli la (ma)tembele la kuchemshwa kwa nyanya na kitunguu. Bila kusahau pilipili shamba.
Hakika hapa ni utamu, na tena ule wa asili kabisa ,yamu yamu yamu....NAWATAKIENI WOTE SIKU /JUMATANO NJEMA SANA.

Tuesday, December 4, 2012

NIMEUPENDA UJUMBE HUU:-)

Nimeupenda ujumbe huu kwa kweli ...nahisi nawe unayesoma umeupenda pia basi ngoja niwatakieni wote mtakaosoma siku njema.PAMOJA DAIMA...

Monday, December 3, 2012

HIVI NDIVYO HALI YA HEWA ILIVYOKUWA FINLAND LEO!!!

Hali ya leo Finland...hapa kwetu bado haijaangua kihivyo ila kuna baridi kali sana kiasi kwamba ile kutoka tu nje pua inasinyaa kabisa....Mwaka huu itakuwa kali kwelikweli...JIONI NJEMA KWA WOTE.....

MWANAFUNZI ABAKWA MPAKA ANAPOTEZA FAHAMU MKOANI RUVUMA!!!

JESHI LA POLISI mkoa wa Ruvuma limefanikiwa kumtia mbaroni Daud Ndunguru (19) wa mtaa wa Hoahoa uliopo Mbinga mjini na linaendelea kumsaka na mwingine jina lake ambaye halikufahamika mara moja linaendelea kumsaka kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa kike wa umri wa miaka 12 (jina lake limehifadhiwa) anayesoma darasa la nne katika moja ya shule za msingi zilizopo Mbinga mjini na kumsababishia maumivu makali na kupoteza fahamu.

Habari zilizopatikana jana mjini hapa ambazo zimethibitishwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma Deusdedit Msimeki zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea desemba 2 mwaka huu huko katika mtaa wa Kihaha nje kidogo ya Mbinga mjini ambako mwanafunzi wa kike inadaiwa alibakwa na watu wawili akiwemo Daud Ndunguru ambaye alikamatwa muda mfupi baada ya kumfanyia kitendo cha kinyama msichana huyo na mwenzake ambaye jina lake halikuweza kufahamika alikimbia na kutokomea kusikojulikana.

Habari zaidi za tukio hilo zimefafanua zaidi kuwa watu hao wawili akiwemo Ndunguru majira ya saa 4:30 usiku walimvizia njiani msichana huyo na kumlazimisha atoe nguo alizokuwa amevaa na kisha kumfanyia kitendo cha ubakaji jambo ambalo limesababisha msichana huyo kupata maumivu makali sehemu za siri na kusababisha kupoteza fahamu.

Hata hivyo kamanda Msimeki alisema kuwa kufuatia kuwepo kw purukushani hizo majirani watoka na kwenda kwenye eneo la tukio ambako walifanikiwa kumkamata Ndunguru na mwenzake alikimbia huku msichana huyo akiwa amepoteza fahamu na walimchukua na kwenda nae kituo cha polisi cha kati cha polisi ambapo walichukua hati ya polisi ya matibabu (PF3) na kwenda nae hospitali ya serikali ya wilaya ya Mbinga ambako amelazwa na anaendelea kupata matibabu na hali yake inaendelea vizuri.
Kamanda Msimeki alisema kuwa mtuhumiwa Ndunguru anatarajiwa kufikishwa mahakamani pindi upelelezi wa tukio hilo utakapo kamilika na jeshi la polishi mkoani Ruvuma linaendelea kumsaka mtuhumiwa mwingine wa tukio hilo anayedaiwa kukimbia na kutokomea kusikojulikana baada ya kumfanyia kitendo cha kinyama msichana huyo
Habari hii nimeipata hapa

Saturday, December 1, 2012

SIKU YA LEO NIMEKUMBUKA LUNDO MBAMBA BAY 2007

Hapa kutoka kushoto ni kaka yangu wa mwisho Philoteo, katikati ni mjomba wangu mwl. John Bosco Ngonyani anajulikana zaidi kwa jina la JB na mwisho ni mwenyewe Kapulya. Siku hii ilikuwa siku ya furaha sana katika maisha yangu kwani nilikuwa sijaonana na mjomba wangu mpendwa karibu mika ishirini ...Muwe na  WAKATI MZURI PIA JUMAMOSI NJEMA YA MWEZI HUU WA KUMI NA MBILI AMBAYO NI YA KWANZA  NA KESHO NDO TUNAANZA KUSUBIRI ULE UJIO /KUZALIWA WA/KWA BWANA YESU KRISTU.

Neno La Leo: Fikiri Kuwa, Sayari Tunayoishi ( Dunia) Ni Jehenamu Ya Sayari Nyingine..​.!

Ndugu zangu,

Kwamba kuna viumbe kwenye sayari nyingine wenye kukesha wakiomba kwenye nyumba zao za ibada, kuwa Mungu wao awaepushe na balaa la kuwaleta kwenye sayari dunia. Dunia iliyo zaidi ya tambala bovu. Dunia iliyojaa wanadamu wenye roho za wivu, kinyongo, inda, husda na nyinginezo. Wanadamu wenye kutakiana mabaya badala ya mema.

Na mfano ni huyu aliyeomba sana kwa Mungu ashushiwe rehma. Siku moja akashukiwa na malaika. Akaambiwa, kuwa Mungu amepokea maombi yake. Kwamba anamtaka mwanadamu huyu achague jambo moja ili ashushiwe. Na akishachagua moja, basi, Mungu atampa jirani yake mara mbili ya kitu alichochagua.

Mwanadamu yule akamwambia malaika; " Basi, niache kwanza nitafakari". Baada ya kutafakari kwa muda,mwanadamu yule akatamka; " Namwomba Mungu anipe chongo!" Kwamba kwa vile alimwonea kinyongo jirani yake apate mara mbili ya atakachokipata, mwanadamu yule aliona ni heri Mungu amtoboe jicho lake moja, awe chongo, na jirani yake atobolewe mawili, awe kipofu!

Naam, fikiri kuwa sayari tunayoishi yaweza ni jehenamu ya sayari nyingine. Kumbuka, nimesema fikiri, hivyo basi fikiri kwa bidii...yaweza kukusaidia kupata jibu la kwanini nchi yetu ni masikini, na watu wake pia.

Na hilo ni Neno La Leo.

Maggid Mjengwa
Iringa.
0788 111 765
Nimetumiwa na http://mjengwablog.com.

Friday, November 30, 2012

TUNAKUMBUKA VIFAA HIVI VYA KUKOBOLEA NAFAKA ZETU TANGU HAPO KALE MPAKA SASA?!!!

Hapo kale kupata ugali uwe wa ulezi, mtama,mahindi au muhogo hiki ndo kilikuwa kinu cha kusagia ili kupata unga. Kama nakumbuka vizuri juzi tu nimeona huko India bado wanatumia kusagia mchele ili kupata unga wa mchele........
 
 Na baadae kikagundulika kinu kwa kukobolea nafaka na pia kupata unga kama vile wa muhogo nk.--
..na baadaye baadaye tukapata mashine ...na mikono ikawa inapumzika kidogo. Sijui  wenzangu mie binafsi nilikuwa mzembe sana hasa kukoboa mahindi. ...je? kuna kifaa kingine zaidi ya hapa unafiri?

Thursday, November 29, 2012

Aina Mpya ya Utapeli Bongo:- Habari ya kweli iliyotokea wiki iliyopita.

Kuna dada mmoja anasoma chuo buguruni na pia ni mfanyakazi hivyo jioni akitoka kazini ndipo huenda shule.Sasa akiwa njiani kuelekea chuo akapigiwa simu na mtu asiyemfahamu akajitambulisha kwamba yeye ni daktari wa lugaro hosp na kumuulizia habari za mwanae ambae alishawahi kwenda kumtibu pale na chakushangaza zaidi akataja mpaka aina na rangi ya nguo aliyovaa siku ile alipokwenda hapo hospitali na yote yalikuwa kweli.

Na zaidi akamwambia najua sasa hivi unaelekea chuo buguruni na kweli ilikuwa hivyo, lakini mwishoni akamweleza kwamba kuna mambo anataka kujua kujua kuhusu hicho chuo hivyo nae anaelekea huko hivyo akifika tu atamtafuta. Kwa muda wote huo huyo dada hakuweza kabisa kumkumbuka ila akajipa moyo kwamba yamkini huyo mtu atakuwa anamfahamu vizuri.

Baada ya kutoka chuo akiwa na wenzake watatu akawa anawasimulia habari za huyo mtu ndipo simu yake ikaita,kupokea yule mtu akamwambia akuona uko na wenzio wawili mnavuka barabara na kumueleza jinsi alivyovaa sasa wenzie wakasema huyo mtu anakufahamu haiwezekani hapa tupo watatu kweli na ameweza kukutambua. Kisha huyo mtu akamwelekeza mahali alipo ambapo haikuwa mbali na barabara.

Lakini alipomtazama hakumfahamu kabisa, basi akampa mkono kumsalimia, baada ya hapo hakujitambua na zaidi alijikuta yuko maeneo ya chuo kikuu cha DSM akiwa hoi. Kuangalia simu na kila kitu chake kilikuwa salama na hakufanyiwa kitu chochote, kwa bahati kulikuwa kuna ndugu yake anasoma chuo hivyo akawasiliana nae ili kupata msaada ikabidi awahishwe mwananyamala hosp lakini ikaonekana sumu iliyotumika ni kali na dawa yake wanayo regency hosp,hivyo akawahishwa regency na kupata matibabu.

Baada ya ufahamu kumrudia akakuta mtu huyo kachukua pesa zote kwenye mpesa,tigo pesa na bank ( NMB na CRDB) kiasi cha milioni 3, hivyo inawezekana walipompa sumu alitaja password pasipo kujijua.

Na bank walipotazama kwenye ATM Camera waliona picha ya huyo mtu na yeye alimkumbuka vizuri, lakini polisi Kijitonyama wakakiri kwamba kesi hizo sasa hivi zimetokea mara nyingi na huo mtandao ni mkubwa, walipoenda kwenye usajili wa simu walikuta ni huyo huyo na jina lake ndilo alilojitambulisha.Ingawa polisi wameshindwa kumkamata.

Akiwa kituo cha polisi mara huyo mtu akampigia simu akimwambia kumbe wewe ni muoga sana tutakurudishia pesa zako’’. Sasa kumbe wanachofanya wanakuambia tutafutie mtu ambae unahisi ana pesa kuliko hizi halafu tukifanikiwa tutarudisha pesa zako’’ hivyo inawezekana nae kuna mtu anaemjua alifanyiwa hivyo akaamua kumtaja yeye.

JAMANI HEBU SOMENI NA IKIWEZEKANA TUMENI HII TAARIFA TO AS MANY PEOPLE AS POSSIBLE.
Habari hii nimeipata hapa

Hivi Kwa Nini tunacheka?


Kicheko ni njia ya mawasiliano, ambayo yanaonyesha ni ukaribu gani tunao na watu wengine. Hata kama mtu anacheka peka yake, kuna tafiti zinaonyesha kwamba hata ukiangua kicheko mara 30, kama tupo pamoja na watu wengine, kuliko tunapokuwa peke yetu.

Kwa kawaida kicheko kinaonyesha ni upamoja gani gani tunao na wale tunaocheka nao. Ni kinyume na nyani ambao wanacheka tu kwa furaha, kicheko cha binadamu kinaweza pia kumchokoza mtu , kicheko kinaweza kuwa cha dhihaka au hisia nyingine. Kicheko wakati mwingine kinaweza kuwa ni njia ya kupata huruma au huzuni pia.

Inaonekana kwamba sehemu kadhaa katika ubongo zimetawaliwa na kicheko. Mwaka 2001 huko Uingereza katika majaribio yao ya NMR X-RAY waliweza kuona sehemu ndogo ya kulia na kushoto ya paji la uso ilionekema ni zenye vichekesho/utan zaidi, lakini hizo aina za tofauti za utan hazifanyi kazi kwenye ulande moja.

Wakati utani unaposomeka, kwa kupima walakini upande mwingine wa mbele wa paji la nyuso kama ilikuwa ya kuchekesha. Inaonyesha kuna chumba cha tatu cha ubongo juu ya paji la nyuso. Ambayo kicheko kinakuja chenyewe.

Pia inaonyesha kuwa mwaka 1998 huko USA, wakati wao wenye vifaa vya umeme vilimfanya msichana wa miaka 16 bila shida kuangua kicheko. Chanzo Illustrerad Vetenskap nr 15/2010.

Wednesday, November 28, 2012

UPUMZIKE KWA AMANI HUSSEIN RAMADHANI A.K.A SHARO MILIONEA!!


SISI TULIKUPENDA LAKINI MUNGU ALIKUPENDA ZAIDI UPUMZIKE KWA AMANI TUTAKUKUMBUKA DAIMA.

NIMEIPENDA SKETI HII/ MREMBO WA LEO!!!


 
Sketi hii nimeipenda sana ni ndefu na ya heshima ...hii ni mimi!!!!:-)
 

Tuesday, November 27, 2012

MTAZAMO WA MAISHA YA ZAMANI NI TOFAUTI KABISA NA MAISHAYA SASA!!!

Habari hii nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mafanikio nami nimeipenda na nimeona nisiwe mchonyo pia ni vema kujadili kwa pamoja...pamoja daima...
---------------------------------------------------------------------------------------------------------
Kwanini nasema hivyo:-  Nasema hivi nikiwa na maana yake, ni kwamba  zamani maisha yalikuwa mazuri na mepesi na yenye khekima kwa wakubwa na wadogo. Vyakula vilikuwa vingi pesa ilikuwa ina thamani. Ikiwa na maana watu waliishi kwa mapenzi mema tena sana. Watoto wakike walifundishwa jinsi ya usafi, kupika, kujiepusha na vitu vya anasa na kadhalika. Na pia wazee waliwapenda wajukuu wao. Wakati wa jioni walikaa nao wakiota moto wakiwa wanawasimulia hadithi nzuri ambazo zilikuwa na mafunzo na pia watoto waliburudika sana. Pamoja na kuwa palikuwa na uhaba wa huduma za jamii ila watu waliishi kwa kula vyakula asilia, na kutumia dawa za miti shamba....,,, Namalizia kusema MAISHA YA ZAMANI YALIKUWA NI BORA KULIKO YA SASA!!! Napenda kusema tena:- Maisha ya kisasa ni tofauti na zamani kwanini nasema hivyo. Maana yake siku hizi watu sio vijana sio wazee wanapenda mambo ya kisasa NA PIA YA KUIGA. Utakuta  wanavaa mavazi tofauti na zamani, wanapenda anasa sana kuliko vitu vinginne, hawapendi kukaa na watoto wao kama wazee wa zamani, hawapendi vitu asilia....! Je? Kuna ukweli kuwa  maisha ya zamani ni bora? KILA LA KHERI!!!!

Monday, November 26, 2012

MAGUNIA YA MKAA KANDOKANDO YA BARABARA..TUKUMBUKE KUPANDA MITI PIA!!!

Hapa ni magunia ya mkaa kando ya barabara yanasubiri wateja/wanunuzi. Kwa namna hii ongezeko la ukataji miti ya asili kwa ajili ya mkaa linachangia sana uhalribifu wa mazingira sehemu nyingi nchini. Basi afadhali tungekuwa tunakata miti na kupanda tena....JUMATATU NJEMA.

Saturday, November 24, 2012

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWEPO/ISHIA IJUMAA YA JANA TULIPATA WAGENI TOKA NYUMBANI TANZANIA!!!

Hakika siku ya jana ilikuwa siku ya furaha sana kwetu. Kama mzaa vile baba wa nyumba akanipigia simu na kusema nina wageni hapa andaa msosi twaja. Nikafanya hivyo muda si mrefu wakatua nyumbani. Wageni kutoka nyumbani tena NYUMBANI kabisa. Kutoka kushoto ni kaka Ludovick Chahally, katikati ni dada Elizabeth Mahinya wao ni mke na mume..na halafu mwisho ni mimi mwenyewe kapulya:-) Nimesisitiza kuwa wanatoka NYUMBANI kwa vile dada Elizabeth anatoka SONGEA pia MNGONI..tuliongea kingoni we acha tu:-) Ni furaha sana kuonana na watu wa nyumbani na kubwa zaidi mnaotoka mkoa mmoja.

Nawatakieni wote JUMAMOSI NJEMA SANA. NDUGU SI LAZIMA AWE BABA NA MAMA MMOJA. HILO MIE NAAMINI KABISA. TUPO PAMOJA DAIMA.

Friday, November 23, 2012

TUPO PAMOJA NA NAPENDA KUWATAKIENI MWANZO MWEMA WA MWISHO WA WIKI!!!

Nawatakieni wote mtaopita hapa mwisho mwema wa wiki na kumbukeni wote mnapendwa: ngoja tu tumalizie na masai raggae :-)

IJUMAA NJEMA!!!

Wednesday, November 21, 2012

MARA YA MWISHO KULA CHAKULA/MAGIMBI ILIKUWA KIHESA -NJOMBE KWA CHAI YA RANGI

Hapa ni magimbi kabla hajamenywa na ....

....hapa tayari yamemenywa na kuchemshwa tayari kwa kula. Magimbi unaweza kula kama chakula cha asubuhi, mchana au jioni. Ila mimi nimeyatamani sana leo na ningeyale kama chakula cha asubuhi hii ya leo kwa....
.

......kikombe hiki cha chai ya rangi  ila sasa.... haya ngoja nile kwa macho. Je? wewe mara ya mwisho ni lini umekula magimbi?

Tuesday, November 20, 2012

HAPA SIJUI PAPOJE? NAONA HII IWE PICHA YA WIKI HII!!!

Sijawahi kuona watu wakifunga kuku kamba..hapa naona dogo amesha chagua kitoweo cha sijui mchana au jioni?  au labda ndo kapata kitu cha kuchezea? MUWE SALAMA WOTE !!!

Monday, November 19, 2012

JUMATATU HII TUNANZE NA SWALI HILI? NINA KASORO GANI?

Jerome na Sesilia walikuwa wamemaliza miaka mitatu tangu waoane. Jerome alikuwa fundi wa saa. Alikuwa amejenga duka lake dogo nje ya nyumba yao. Kila siku, isipokuwa Jumapili, watu waliweza kumkuta hapo. Alipenda kuimba wakati akifanya kazi na kama hakuwa akiimba, basi redio ilikuwa ikicheza muziki kwa sauti kubwa na safi kwa wapita njia wote kusikia.

Watu waliwafahamu kama watu wawili wenye raha. kabla ya kufunga ndoa, Sesilia hakuwahi kuishi mjini. Miaka yake ya kwanza nyumbani mwao mpya ilimshangaza kwa vile alivyowaona watu wakiharakisha kwenda huku na kule. Katika kijiji chake alimokuwa, maisha yalikuwa tofauti sana na tena ya polepole zaidi. Lakini hapa kelele zilikuwa nyingi mno, milio ya honi hasa za watu wenye taksi, na sauti za watu wakiitana.

Lakini alikuwa anafurahi kuvumilia yote haya kwa ajili ya ndoa yake kwani alimpenda sana Jerome. Alijua ya kwamba Jerome alimpenda pia. Hakuongea sana juu ya jambo hilo, lakini Sesilia aliweza kuliona kwa namna alivyokuwa anamwangalia, katika utaratibu wa sauti yake na katika kumtunza kwake. Alizoea kuimba alipokuwa akifagia nyumba. Huko nje pia Jerome naye alikuwa akiimba na sauti zao kwa pamoja ziliwaambia watu waliopita karibu kwamba hiyo ilikuwa ndiyo nyumba yenye raha.

Siku moja, Sesilia akiwa sokoni, alisikia jambo lililomtia uchungu sana. Lucy, kutoka katika kijiji chake, alimwambia kwamba jioni iliyopita alikuwa amemwona Jerome akiingia katika nyumba ya wageni.

"Kwa nini lakini?" Sesilia aliwaza. "Bila shaka siyo kuwa na mwanamke mwingine" Ndiyo Lucy alikuwa na hakika alikuwa ndiye Jerome. Sesilia alijaribu kujisadikisha kwamba bila shaka haikuwa hivyo lakini hakuweza kufukuza wasiwasi mkubwa uliokuwepo moyoni mwake. Alifahamu kwamba watu wengi kati ya watu wake hawakuona kwamba ni jambo baya sana kwa mtu wa ndoa  kuwatembelea wanawake wengine. lakini aliamini ya kwamba ndoa yao ilikuwa tofauti na ndoa nyingine nyingi.

Aliamua kutosema neno lolote. Atasubiri na kufungua macho. Jerome alionekana kama hali yake ni ya kawaida lakini hapa na pale Sesilia alitambua badiliko katika mwenendo wake kwake. Ama, haya yalikuwa ni mawazo yake tu? hakuweza kusema.
Jioni moja, baada ya chakula cha jioni, Jerome alimwambia Sesilia kwamba alikuwa anakwenda kutembea. "Nimeketi kutengeneza saa kutwa kucha, na nisiponyosha miguu ninahofu nitasahau namna ya kutembea", alimwambia haya haku akifunga mlango wa duka lake.
Alipomfuata nyuma barabarani, Sesilia aliona aibu ya kufanya hivyo. Lakini ilimbidi kujua. Labda alikuwa anakwenda kwa wanawake. Walikuwa wanaelekea kwenye nyumba ambayo Lucy alikuwa amemwelezea. hata hivyo mtu aliyeweza kuwa na sababu nyingine za kutembea kwenye mtaa huu. Labda Jerome hakujali alikuwa anakwenda wapi.

Moyo wa Sesilia ulisimama alipomwona Jerome akiingia kwa mlango wa nyuma wa baa /nyumba ya wageni
maalumu ambayo waliishi wanawake. Kumbe, Lucy alikuwa amesema kweli. Akijawa na uchungu, huzuni na hasira, Sesilia alirudi nyumbani polepole. Alijiuliza: "Nina kasoro gani? kwanini Jerome ana haja ya kumwendea mwanamke mwingine? Kwa nini hakai nami? Nina kasoro gani?"
Sesilia hakuweza kujua kilichokuwemo akilini mwa Jerome. Hakuweza kujua kwamba Jerome alikuwa amezoea raha aliyokuwa nayo na kwamba sasa alitaka kuonja kitu kipya, alitaka kugundua mambo mapya na pia alitaka watu wapya wamtosheleze. Sesilia hakujua hayo lakini aliazimia atamfundisha Jerome asikose uaminifu tena----yaani hata naye Sesilia atapata mpenzi.
Je? Unafikiri nini kilimfanya Jerome afanye kama alivyofanya?


Sunday, November 18, 2012

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE MTAKAOPITA HAPA!!!


Hakuna binadamu aliyekamilika. NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA .

Saturday, November 17, 2012

NAPENDA KUWATAKIENI WOOTE JUMAMOSI HII IWE YENYE FURAHA NA UPENDO!!!!

JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE NA TUKUMBUKANE KWANI SOTE NI WATOTO WA BABA MMOJA. upEnDo DaImA.....!!!!!!!!!!!!

Friday, November 16, 2012

BAADA YA KAZI YA KAZI KWA JUMA NZIMA KWA WENGINE BASI KAA CHINI NA SIKILIZA UJUMBE HUU...NA UWE NA MWISHO WA JUMA MWEMA.....ZILIPENDWA!!!


NAWATAKIENI WOTE IJUMAA NJEMA KUNA WENGI  WATAPUMZIKA MPAKA JUMATATU NA WALE WANAO ENDELEA NA KAZI JUMAMOSI NA JUMAPILI BASI NIWATAKIENI KAZI NJEMA MOJAWAPO NIKIWA MWENYEWE....WOTE MNAPENDWA...KAPULYA

Thursday, November 15, 2012

UJUMBE WA LEO!!!

Kulazimisha/kubembeleza kitu/mtu siyo vizuri ..kama Mungu amepanga basi kitatokea/itatokea tu........
NAWATAKIENI ALHAMIS NJEMA WOTE:-)

Wednesday, November 14, 2012

UMESHAWAHI KUCHEZA MCHEZO HUU?!!

Maisha siku zote huwa tofauti toka ulipokuwa mtoto hadi kufikia uzeeni. Hatua hii hupitia mambo mbalimbali haswa za kimechezo. Nakumbuka nilipokuwa mtoto tulicheza michezo mingi ya heshima tofauti na watoto wa sasa hivi.  Haya yote yanasemekana ni kutokana na utandawazi ambao huwajengea watoto ufahamu zaidi.
Huu ni mchezo wa Kuruka kamba ambao tuliucheza utotoni na pia kiafya una umuhimu. Michezo mingine ni Kombolele(Mchezo wa kujificha), Utengenezaji wa magari, Ndege wakati wa mavuno, Midoli ya kutengeneza,  Kula mbakishie baba, Kutengeneza vitu mbalimbali kwa kutumia udongo, ukutiukuti, Kioo Kioo, mdako mpira (lede ledesta) ,Kujipikilisha....................................pia katika mchezo huu wa kuruka kamba nakumbuka tulikuwa tukiimba  hivi:- Kamwambie baba baba sisi tunacheza cheza hatuogopi fimbo fimbo mtoto acha kuningínikax2.....
Sijui ndo uzee naona kama nimesahau basi tusaidiane kukumbushane ......!!!!!!!!
Tafakari juu ya mtoto wako ingawa sasa hivi tunawanunulia vitu vya kuchezea ila wanavitumia ipasavyo na halafu vinakuwa vingi mno. Nimekumbuka sana michezo hii ya utotoni ..je? nawe unakumbuka kitu?
MAISHA NA MAFANIKIO INAWATAKIA WOTE JUMATANO NJEMA SANA!!! DAIMA PAMOJA.




Tuesday, November 13, 2012

NIMEONA TUBAKI KIDOGO HAPA SONGEA:- HAPA NI PIKIPIKI KWA AJILI YA KUWABEBA AKINA MAMA WAJAWAZITO KATIKA HOSPITALI YA MKOA WA RUVUMA!!!!


Nimeupenda ubunifu huu, labda unaweza kuokoa maisha ya akina mama wengi....
Hizi ni pikipiki maalumu kwa ajili ya kubebea wajawazito toka maeneo ya vijijini na kuwafikisha hospitalini.
Nimependa hii kwa kweli kwasababu wajawazito huwa wanapata taabu sana na mwishowe hufa au mtoto kufa.

Monday, November 12, 2012

TURUDI TENA SONGEA KWETU:-UVUNAJI WA MITI KATIKA MILIMA YA MATOGORO KWASABABISHA KUKAUSHA MTO RUVUMA!!!

Na Daniel Mbega, Songea
 MVUA zilikuwa zikimtendea haki Josephat Komba, mkulima katika kijiji cha Ndilima Litembo wilayani Songea, wakati pepo za kusi zilipovuma vyema na hivyo shamba lake la mpunga kupata maji ya kutosha yaliyompa mavuno mengi. Lakini hana uhakika kama atapata bahati kama hiyo msimu ujao.
“Zamani, hatukuwa na mashaka kuhusu hali ya hewa,” anasema Komba, akiwa shambani kwake kilometa kadhaa kutoka Songea mjini. “Lakini hivi sasa, tatizo ni kubwa mno.”
Komba anaitazama Milima Matogoro kwa masikitiko, na kujiuliza kama mabadiliko hayo ya hali ya hewa yameletwa na Mungu au wanadamu.
“Tumesikia mara kadhaa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, lakini nikwambie ukweli, miaka ya nyuma milima hii unayoiona hapa ndiyo ilikuwa mkombozi wetu. Tuliitegemea sana kwa ajili ya kuleta mvua, sasa hatujui kama ni laana ya Mungu au ni binadamu ndio tunaosababisha majanga haya,” anasema.
Komba anasema, zamani walikuwa wakipanda kwa wakati na mvua zilinyesha katika kipindi kile kile. “Lakini tangu walipoanza kufyeka miti kwenye milima hii, kila kitu kimebadilika. Nadhani wameikasirisha miungu.”
Misimu kadhaa iliyopita, mvua zikaanza kuadimika. Mara kadhaa mpunga wake ulikomaa bila unyevu; karibu theluthi ya mimea yake ilikauka kwa ukame na hata Mto Ruvuma ambao amekuwa akiutegemea umekuwa hauna maji ya kutosha hata nyakati za masika.
Mabadiliko hayo ya ajabu ya hali ya hewa ndiyo ambayo wanasayansi wa mazingira wanaamini kuwa ni madhara ya mabadiliko ya hali ya hewa. Wakati mwingine kunaweza kuwa na ukame, lakini msimu mwingine mvua zinaweza kuwa nyingi kiasi cha kuleta mafuriko hivyo kushindwa kulima.
Komba analalamika kwamba, uchomaji wa moto kwenye msitu wa milima hiyo ni sababu nyingine inayoondoa hali ya asili ya milima hiyo ya Matogoro na hivyo kuleta wasiwasi mkubwa kwamba mito mikuu kama Ruvuma, Luhira na Luwegu itatoweka katika miaka michache ijayo.
Sehemu kubwa ya msitu wa Milima ya Matogoro imebakia vipara kutokana na uvunaji wa miti ya kigeni (exotic trees) kama Misindano (Pines) na Mikaratusi (Eucalyptus) ambayo wataalamu wa hifadhi ya vyanzo vya maji wanasema inayonya maji mengi.
Mhandisi Jaffari Yahaya wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Manispaa ya Songea (SOUWASA) anasema kwamba kuwepo kwa ukosefu wa maji wakati wa kiangazi katika Manispaa ya Songea kunachangiwa kwa kiasi kikubwa na aina ya miti ambayo ipo katika misitu ya milima Matogoro ambayo hunyonya maji kwa kiwango kikubwa kwa kipindi cha mwaka
Soma zaidi hapa

TUANZE JUMATATU HII KIHIVI ...JUA...!!!

Sikumbuki ni lini nimeona jua likichomoza kama hili hapa. Au sijui linazama hapa? kama ule wimbo wa mchaka mchaka.....Jua lile litelemke mama ...litelemke mama litelemke....mmmhhh ila hapa naona linachomoza angalia tu mionzi yake,,,au Wenzangu mnasemaje?...Haya JUMATATU NJEMA...!!!

Saturday, November 10, 2012

JUMAMOSI YA LEO NAPENDA KUSEMA:- AHSANTE MAMA MUNGU AKUPE KHERI DAIMA!!!

 
AHSANTE MAMA MUNGU AKUPE KHERI DAIMA
 
Nimeyapenda maandishi haya kwenye kanga hii na hapa si kwa ajili ya mama yangu tu nawaombeni wote ambao mnaweza kuwashukuru akina mama basi chukueni nafasi hii na kuwashukuru kwani
HAKUNA KAMA MAMA. JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE!!! NIPO  NANYI!! 

 

Friday, November 9, 2012

UJUMBE WA IJUMAA YA LEO NI:-.......

Riziki ni mdudu popote hutua!
MUWE NA IJUMAA NJEMA NA MWISHO WA JUMA MWEMA....KAPULYA!!!

Wednesday, November 7, 2012

NIPO INGAWA SIPO ILA NIPO!!!!

Kutokana na taarifa niliyowapa hapo jumapili basi ndiyo maana nitakuwa kidogo sionekani sana hapa ila nipo na pia napenda kutoa SHUKRANI ZA DHATI kwa wale wote waliuotufariji. TUPO PAMOJA NA MUNGU AWAZIDISHIE UPENDO. MUWE SALAMA WOTE!!!

Sunday, November 4, 2012

JUMAPILI YA LEO NAPENDA KUSALI SALA HII KWA MAREHEMU WOTE AKIWEPO MAMA MKWE WANGU AMBAYE KATUACHA JANA!!!

Na tuwaombee marehemu
Ewe Baba Mwenyezi, Mpaji wa maisha na afya, twakuomba uwaangalie kwa rehema marehemu pia wagonjwa wote, hasa wao wanaotakiwa maombi yetu, ili kwa baraka yako juu yao, na juu ya wao wawatumikiao, ikiwa mapenzi yako warudishiwe afya yao ya -mwili na ya roho,na pia marehemu wote wastarehe kwa amani, nao wakutolee shukrani katika kanisa lako takatifu; kwa Yesu Kristo, Bwana wetu. Amina.
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE NA UPENDO UTAWALE NDANI YA MIOYO YENU.

Friday, November 2, 2012

NAPENDA KUWATAKIENI MWANZO MWEMA WA MAPUMZIKO !!!

There some place in this world maybe left to be unvisted, there som worlds maybe left to be unsaid, there some story maybe left to be unnarrated, but the special one as you, you will never left to be unrembered. WOTE MNAPENDWA SANA NA IJUMAA /MAPUMZIKO MEMA KWA WOTE.
EBU PILIPILI&KELMA WAMALIZIE NA UGALI....

PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA......!!

Wednesday, October 31, 2012

TUTEREMKE KIDOGO MPAKA SONGEA MJINI SASA:- TATIZO LA MAJI NA PIA MAFUTA KUADIMIKA!!!

Tatizo la maji Songea mjini, ndoa moja ya maji shilingi 500....
 
Na hapa ni madereva wa pikipiki katika foleni ya mafuta hapa ni kituo cha mafuta cha Kisumapai. Ni kwamba sasa imefikia mafuta yanatolewa kwa mgao Songea yetu....Natumaini matatizo haya yataisha karibuni kwani vitu hivi vyote ni muhimu sana katika maisha ya binadamu.

Tuesday, October 30, 2012

SIKU YA MAHAFALI KATIKA SEKONDARI YA WILIMA/MADABA/MATETEREKA=SONGEA!!!!

Kutoka kushoto ni Meneja wa shule ya sekondari Wilima mzee Lucas Mayemba, katikari ni Mwl.Paul Mgaya wakati sisi tunaishi hapa alikuwa  mkuu msaidizi.  Hapa wapo katika jengo la utawala katika shule hiyo na mwisho hapo ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Songea Bw. Rajabu Mtiula
 
 Mmoja wa Wahitimu akipokea Cheti cha kuhitimu kidato cha nne....Ni furaha ilioje kuweza kufika hapa tena ingwa kipicha. Nimefurahiiiiii sanaaaaa hasa kuwaona mzee Mayemba na  Mgaya PHD......Hapa ndipo nilipoanzia MAISHA YANGU. Picha http://mwambije.blogspot.se/ nakushukuru sana uliyepiga picha.

MIKUMI NATIONAL PARK/MBUGA YA HIFADHI YA WANYAMA MIKUMI 2011 MWEZI WA SITA!!!

 Jamani subirini kwanza sisi tupite...Nyani/tumbili hao walivyojua kuziba njia
 Hakuna mnyama mzuri kama twiga...habari jamani!!!
Tulipata bahati ya kumwona Nyati  pia mnyama asemekanaye mwenye hasira kuliko wote..Kwa mbele ni hawa Funo hawa hukosi kuwaona ukifika /pita Mikumi

Monday, October 29, 2012

HUYU NDIYE YASINTA NGONYANI!!!

Nimeamka leo na mawazo mengi sana kichwani mwangu kuhusu huyu mdogo wangu wa hiari Koero Mkundi. Sijawasiliana naye kwa muda sasa nafikiri yupo salama. Baada ya kufikiri sana nikakumbuka mada hii nikaona ngoja niiweka hapa ni kumbukumbu kubwa sana kwangu.

Yasinta Ngonyani, Picha kwa hisani ya Maisha Blog
Ni binti halisi wa kitanzania, ingawa anaishi ughaibuni lakini hujivunia asili yake na utaifa wake, ni binti pekee aliyejitolea muda wake kuwaelemisha watu wa rika zote bila kujali rangi, kabila, itikadi, taifa wala jinsia.

Binti huyu si mjivuni na hupenda kubadilishana mawazo na watu mbali mbali, na pia hupenda kufuatilia habari za nyumbani kwao alikotoka na haoni tahayari kuongea lugha ya kwao. Daima hujitambulisha kwa jina la asili ya kwao na huona fahari kutumia jina hilo.

Binti huyu hakuona ajizi kuwajuza wanae asili ya kwao japo wamezaliwa ughaibuni, amekuwa msitari wa mbele katika malezi ya wanae ili kuhakikisha wanae hao hawajitengi na asili ya aliotoka yeye.

Si mchoyo wa ushauri na kupitia makala zake aziwekazo kibarazani kwake amekuwa ni msaada kwa wengi, amekuwa mstari wa mbele katika kuilemisha jamii bila kujali rika. Amejitolea kufundisha kile akijuacho juu ya malezi na matatizo mbali mbali yanayowakabili wanandoa na malezi ya watoto.

Kibaraza chake kimekuwa ni kitovu chenye kukutanisha wadau mbali mbali wenye fikra pevu, na kuibua mijadala yenye kuelimisha, kufundisha, kuburudisha na kuhuzunisha pia.

Binafsi napenda kumuita dada na kwangu mimi ni zaidi ya dada, kwani amekuwa ni mwalimu mzuri kwangu nikijifunza mambo mengi kupitia kibaraza chake nimekuwa nikijifunza mengi, na sisiti kukiri kwamba chimbuko la kibaraza cha VUKANI ni kutokana na kile nilichojifuza kwake.

Ni mkweli na muwazi, na hasiti kusema wazi hisia zake, lakini huwa makini sana ili kuepuka kumuumiza mtu mwingine kihisia, na kama kwa kusema huko kutamkera mtu mwingine, ni mwepesi kuweka sawa maelezo yake ili kuondoa msigishano wa mawazo.

Nakumbuka wakati fulani nlipopata msongo wa mawazo kutokana na tofauti zangu na wazazi wangu, alikuwa ni mtu wa kwanza kunitumia email binafsi akijaribu kuniliwaza na kunitaka nisichukue hatua yoyote kujidhuru, naomba nikiri kwamba email ile ilinisaidia sana kurudi katika hali yangu ya kawaida na nilijisikia fahari kuona kwamba kuna mtu ananipenda na kunijali japo sijawahi kuonana naye uso kwa uso.

Huu kwangu ulikuwa kama muujiza, inakuwaje, mtu kusoma mawazo yangu kupitia blog tu halafu awe karibu nami kiasi hiki, ni kitu gani kimemvuta? Kusema kweli tangu siku hiyo niliamni kuwa maandishi yana nguvu sana na kupitia maandishi yawezekana mtu mwingine kukufahamu vizuri sana.

Nimekuwa karibu sana na binti huyu, na amekuwa ni mwema sana kwangu na mshauri wangu pia, na kupitia vibaraza vyetu, tumekuwa tukibadilishana mawazo na kupeana ushauri mbali mbali ili kuboresha ustawi wetu na wa familia zetu.
--------------------------------------------------------------------------
KOERO HUKO ULIKO MUNGU AKULINDE NAKUKUMBUKA SANA KILA SIKU UWE SALAMA.


NI JUMATATU YA MWISHO YA MWEZI HUU NAMI NIMEONA TUIANZE HIVI!!!NIMEUPENDA WIMBO/UJUMBE HUU KUHUSU KUPENDA UNAWEZA KUSIKILIZA UKIPATA WASAA!!!


JUMATATU NJEMA KWA WOTE!!

Sunday, October 28, 2012

NAPENDA KUWAYTAKIENI WOTE JUMAPILI HII YA MWISHO WA MWEZI HUU IWE NJEMA SANA!!

Leo ni Jumapili ya mwisho wa mwezi huu wa kumi nami nawatakieni wote Jumapili njema sana binasi itaishi kubeba mabox...JUMAPILI NJEMA KWA YOYOTE ATAKYEPITA HAPA NA KUSOMA UJUMBE HUU.

Thursday, October 25, 2012

UNATAKA KUNYWA SODA/VINYWAJI BARIDI? BASI JARIBU NA HII HAPA/AKILI NI NYWELE KILA MTU ANA ZAKE-UBUNIFU!!!

JIPATIE VINYWAJI BARIDI

Kuna namna nyingi ambazo sisi wanadamu tunaweza kujipatia huduma zetu tofauti na vile tulivyozoea. Ili kinywaji kiwa baridi tumezoea kukiweka kwenye jokofu/fridge ili kipate baridi, na hii hutumika zaisi maeneo yenye hali joto kama vile Dar Es salaam nakadhalika. Kwenye sehemu za baridi kwa Tanzania kama vile Njombe, Mufindi, Makambako n.k mara nyingi hawatumii majokofu, kwa kuwa vinywaji hivyo vinakuwa vya baridi tayari.
Sasa basi iwapo huna jokofu haimaanishi huwezi kujipatia kinywaji cha baridi. Ni hivi chukua soda na uziweka ndani ya maji yaliyomo ndani ya mtungi kwa usiku mzima, na asubuhi zinakuwa baridi  safi kabisa kwa kukata kiu yako.
Vyungu hivi hutengenezwa na sisi wenyewe waTanzania, na hutumika kwa matumizi ya kupikia, kuhifadhia na leo hii tunajifunza pia twaweza kufanya zoezi hili. Pia kuna aina nyingine ya ubunifu katka kutaka kinywaji kiwe baridi ni hivi:- Chukua soksi na uiweke chupa ndani ya soksi na halafu weka maji kwenye chombo chochote kile kama ndoo vile utaona matokeo yake itakuwa baridiiiiii..UJANJA eehh:-)

SI MWINGINE TENA BALI NI NURU WETU AMEFANYA TENA KILE ANACHOKIWEZA...HAYA EBU MSIKILIZE HAPA HUU WIMBO MPYA CHAPA LAPA!!

Nachukua nafasi hii na kumpongeza dada Nuru kwa kazi nzuri aliyoifanya.Ni ujumbe mzuri kama una muda sikiliza ...chapa lapa kaka sitaki tena mapenzi kila siku unachanganya danganya  danganya toto ..aahhh sikiliza mwenyewe...

Kila la kheri !!!

Wednesday, October 24, 2012

HIVI LINI UMECHEKA AU KUTABASAMU BASI UNGANA LEO NAMI KUHUSU HILI: Maongezi ya Mtoto na Baba'ke

Baba: We mtoto hebu niletee soda...
Mtoto: Cola au Pepsi?
Baba: Pepsi.
Mtoto: Kopo au Chupa?
Baba: Kopo.
Mtoto: Baridi au moto?
Baba: Baridi.
Mtoto: Ndogo au Bonge?
Baba: Aaa! Basi niletee tu maji.
Mtoto: Ya bombani au dukani?
Baba: We mtoto nitakupiga?
Mtoto: Na mti au chelewa?
Baba: N'takuua nakwambia!
Mtoto: Kwa kudu au bunduki?
Baba: Bunduki.
Mtoto: Kichwani au kifuani?
Baba: Mbaff, toka nje!
Mtoto: Sasa hivi au baadaye?
Baba: Sasa hivi.
Mtoto: Kwa hiyo maji hutaki tena?
Baba: (kimoyomoyo) "nilimwambia mke wangu tukilewa tusifanye, yeye anang'ang'ania, haya ndiyo matokeo yake..."
Source: http://www.wavuti.com

Tuesday, October 23, 2012

NIMEIPENDA PICHA HII NA NIMEONA IWE PICHA YA WIKI/WAREMBO WA WIKI!!!

 
Kwa kweli nimeipenda hii picha hebu iangalie wewe unaona nini katika picha hii? ukitaka kumsoma zaidi mdada huyu basi bonyezaga hapa...

WIKI HII NAONA ITAKUWA YA RUVUMA---TURUDI SONGEA TENA..


Wote tunajua MAJI ni muhimu kwa uhai wa binadamu ...kuwa na maji safi na salama kila mtu ana haki lakini si wote wanapata huduma hii...KILA LA KHERI

Monday, October 22, 2012

TUSIISHIE SONGEA NGOJA TUENDELEE MPAKA KWETU NYASA:- HIZI NI TASWIRA ZA NYASA

 
MAWINGU HAYO SIJUI NDIO MWANZO WA KUCHAFUKA ZIWA?
 
NA HAPA HAKUNA  HAKUNA TAABU YA KUSUBIRI SANA SAMAKI NI KUINUKA TU..PIA MAJI KARIBU ...naimekumbuka sana nyasa....

TUANZE JUMATATU HII KWA KUTEMBELEA KIJIJI FULANI SONGEA!!!

Kwa wale wanaotoka Songea au wale waliofika Songea hivi hapa ni wapi? Ni kijiji gani hiki? Jumatatu njema kwa wote

Sunday, October 21, 2012

NAPENDA KUWATAKIA WOTE JUMAPILI NJEMA NA MAPUMZIKO MEMA!!!

Akamwambia mwanamke, hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako kwa uchungu utazaa watoto na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala. Mwanzo 3:16
JUMAPILI/DOMINIKA IWE YENYE UPENDO.

Saturday, October 20, 2012

Neno La Leo: Hakuna Ugumu Wa Kurudi Misri...

Habari hii nimetumiwa na kaka Mjegwa.....
-------------------------------------------------------------------------------------
Ndugu zangu,
Yanayotokea katika nchi yetu kwa sasa yanatutaka tufikiri kwa bidii. Kama nchi kuna safari tumeifunga. Na tulivyo Waafrika, tu mahodari wa kufunga safari, lakini si mahodari wa kupanga safari. Kufunga na kupanga safari ni vitu viwili tofauti.

Ndugu zangu,

Ni vigumu leo kwa Wana wa Israel kuamua kurudi tena Misri, hata kama, pamoja na chawa na kunguni walioaacha Misri, bado, kuna wanaokumbuka samaki na masufuria ya pilau waliyoayaacha Misri. Lakini, kijamii, na kwa kuingalia jamii yetu hii ilikotoka, ilipo sasa na inakoelekea, na tuone sasa, kuwa hakuna ugumu wa kurudi tena Misri. Na hapa nitazungumzia umuhimu wa sisi WaTanzania kujitambua.

Nahofia, kuwa moja ya kiini ya haya yanayotukuta sasa ni dhambi ya Ubaguzi iliyoanza kututafuna pole pole. Taratibu tunapoteza uwezo wetu wa kujitambua. Ni ukweli sasa, kuwa Watanzania hatujitambui, na kibaya zaidi, baadhi ya viongozi wetu wa kisiasa na kidini wanapoonyesha wazi wazi kuwa hawajitambui.

Maana, tumeanza sasa kuzungumza lugha za ' Wao Wakristo' na ' Sisi Waislamu'. Tunasahau, kuwa sisi ni ndugu wa damu. Kuwa SISI ni Watanzania Kwanza. Na lililo la kwanza kwetu ni ' Nchi Yetu' na maslahi yake.

Hii ni Nchi Yetu Sote. Kila Mtanzania kwa nafasi yake ana lazima ya kupigania Usalama wa Taifa letu. Usalama wa Nchi Yetu tuliyozaliwa. Hatuwezi kuilinda na kuijenga Nchi Yetu kwenye mazingira ya kubaguana. Kwenye mazingira ya kugawanyika kwa misingi ya udini, ukabila na rangi. Na hapa nitamrejea tena Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na dhana ya Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa.

Ni Mwalimu Nyerere aliyeuanzisha na kuusimamia mradi mkubwa wa Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa, hata hivyo, tunaona sasa unavyoporomoka na kuliacha taifa letu mashakani. Ndio, Mwalimu alijenga misingi imara ya Ujenzi wa Umoja Wa Kitaifa ( Nation Building).

Kuijenga jamii ya Watanzania yenye kuamini kwenye ukweli kuwa sisi sote ni ndugu. Kwamba Nchi yetu haina dini. Yenye kupiga vita ubaguzi wa aina zote, iwe wa rangi, kabila au dini. Ilimchukua Mwalimu na taifa letu miaka mingi sana kuijenga misingi hiyo iliyowawezesha pia Watanzania kuwa na mioyo ya uzalendo kwa Taifa lao.

Tunaona sasa, kazi hiyo iliyochukua miaka mingi, kutokana na ubinafsi na uroho wa madaraka ya baadhi ya wanasiasa wetu, wanapelekea kubomoka kwa misingi hiyo na kuliacha taifa letu kwenye hatari ya kuangamia.

Ndio, msingi wake ni ubaguzi wa kisiasa unaotokana na ubinafsi na tamaa ya mali kwa baadhi ya tuliowapa dhamana za kufanya maamuzi makubwa kwa niaba yetu. Ni hali ya baadhi ya tuliowapa dhamana za uongozi kuishiwa chembe chembe za uzalendo; mapenzi kwa nchi yao.Ni watu wenye kulinda maslahi yao na ya wanaowazunguka. Wako tayari hata kutumia mbinu za Umafia kutimiza malengo yao. Kuna Watanzania wengi sasa wanaopoteza mioyo ya uzalendo kwa nchi yao.

Kuna hata wenye kufikia kutamka; 'Nchi hii ina wenyewe'. Kuna anayetamka hilo kwa lengo la kumtishia mwenzake au kulazimisha kitu fulani kifanyike. Lakini, kuna wenye kutamka hivyo kuashiria kukata tamaa. Kuwa hata wafanye nini, hakuna anayewasikiliza ama kuwajali. Hizi si dalili njema kwa taifa. Kuna wanaoiba mali ya umma mchana wa jua kali. Hakuna anayewagusa.

Ukiuliza utajibiwa; “Ah! Nchi ina wenyewe!”. Kwamba kuna baadhi yetu hawajisikii kuguswa na nchi hii, hawajisikii kuwa na nguvu ya kupiga vita maovu yanayotusumbua. Baadhi yetu wameanza kupungukiwa na mapenzi na nchi yao.

Juni 16, 2004 nilipata kuandika hili kwenye gazeti la Majira; kuwa Tanzania ina vyote, kasoro Watanzania. Niliandika; kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana. Ni nchi ya kujivunia. Kwamba Tanzania ni nchi kubwa sana kwa eneo. Ni nchi yenye rasilimali nyingi; ardhi yenye rutuba, mito, maziwa, milima, mabonde, bahari na vivutio vingi vya asili.

Hata hivyo, Tanzania ni moja ya nchi masikini sana duniani. Kwa nini? Ndio, kikubwa kinachokosekana Tanzania ni Watanzania. Tanzania tunayoijenga sasa ni mkusanyiko tu wa watu wa makundi mbali mbali wenye kwenda kwa staili ya 'kila mtu na lwake'. Idadi ya Watanzania wenye uzalendo na mapenzi kwa nchi yao inazidi kupungua. Ubinafsi umekithiri, na ubinafsi mbaya zaidi ni ule wenye kufanywa na viongozi.

Ndugu zangu, Hakuna ugumu wa kurudi Misri. Tuna lazima ya kupanga safari ya kurudi tena Misri. Inawezekana.

Na hilo ni Neno la Leo.

Maggid Mjengwa,

Iringa,

0788 111 765, 0754 678 252
http://mjengwablog.com

Friday, October 19, 2012

DAR ES SALAAM /KARIAKOO HAKUNA AMANI LEO HII

Mwenyezi Mungu nakuomba uzidi kuiongezee Tanzania yetu ili kusizidi zaidi ya hapa. Watu wawe na upendo na amani kama mwanzo..MUNGU IBARIKI TANZANIA YETU PIA WATU WAKE....