Friday, May 17, 2013

TUSISAHAU USEMI/SEMI WETU/ZETU..LEO TUANGALIA HUU UFUATAO......!!!

Dunia/Ulimwengu ni kama kitabu, na wao waisosafiri, wanasoma ukuraza mmoja tu.
NAWATAKIENI MWANZO MWEMA WA MWISHO WA JUMA.TUKUMBUKANE:-)

Thursday, May 16, 2013

MAANDALIZI YA BUSTANI ZA MBOGA NA MAUA YAMEANZA...ANGALIEANI WENYEWE...KARIBUNI TUJUMUIKE!!!!

 Hapa ni baadhi ya matu ya bustani yangu ...maandalizi yameanza..leo mnaona udongo tu hapa baada ya wiki mtaona mimea....
 Katika maisha inabidi uwe mtundu hapa nilikwisha andaa baadhi ya miche kama vile NYANYA na Miche ya mboga ZA MABOGA,,ujanja eeeehhh
Mdada/kapulya hapendi shughuli za bustani za mboga tu ni mpenzi sana wa bustani sana wa bustani za maua kama mnavyoona hapa na mawe pia....kwa hiyo msione nipo kimya nipo ...daima pamoja...anayejisikia kuja kusaidia anakaribishwa..majembe yapo mengi tu:-)

Tuesday, May 14, 2013

WANANDOA NA KAULI HIZI: HATA VIKOMBE KABATINI HUGONGANA, ITAKUWA SIE?

Je unadhani au kuamini kwamba kuna ndoa ambazo wanandoa wake hawagombani kabisa? Kama unaamini hivyo, basi unajidanganya na labda unaishi katika dunia ya peke yako.
Ni jambo lenye ukweli wa kutosha kabisa kwamba wanandoa wote duniani hutokea kugombana, lakini kugombana huko hutokana na migongano au mizozo ya muda tu ambayo huweza kutatuliwa na pande mbili kama wakiamua kufanya hivyo.
Wewe unayesoma hapa, napenda kukuambia ukweli kwamba usiogope migogoro ya ndoa, kwani hicho ni kitu ambacho kamwe huwezi kukiepuka. Kuna msemo mmoja unatumika sana huko nyumbani usemao, " hata vikombe kabatini hugongana itakuwa wana ndoa?" Hii ina maana gani, ina maana kwamba haiwezekani watu kuishi pamoja halafu msiwe mnatofautiana, na kama ukiona hivyo, jua kwamba hiyo ndoa si salama kwani siku yoyote bomu litapasuka na madhara yake yatakuwa ni makubwa kuliko kawaida.
Kuna watu ambao hata kama wamekosewa na wenzi wao hunyamaza kimya na kumeza hasira zao, wengine huogopa kuwakabili wenzi wao na kuzungumzia jambo linalowakera kwa kuhofia kuonekana kama wana kasoro au ghubu. Jambo hili ni hatari sana.
Kumkabili mwenzi wako na kumwambia hisia zako kama amekukosea au amekwenda kinyume na matarajio yako ni jambao la maana sana katika kudumisha uhusiano. Lakini naomba nitahadharishe kwamba, ni vyema kufanya hivyo bila kumshusha, kubeza au kusimanga kwani hiyo sio dalili nzuri ya upendo.
Inashauriwa kwamba wanandoa au wapenzi wanapokwaruzana inabidi wajadili tofauti zao bila kusigishana, kila mmoja akitaka kuwa mshindi, hiyo haitasaidia kuimarisha ndoa bali itaongeza tatizo. Ni vyema upande unaohusika na tatizo, uwajibike na kuomba radhi kwa ustawi wa ndoa, huo ndio ukomavu.

Kutojadili mgogoro kwa wanandoa na kuupatia ufumbuzi wa tatizo huwafanya wandoa kuwa mbali kihisia, na athari zake ni kuwakuta wanandoa wakiwa wageni wa kila mmoja kwa mwenzake, yaani hakuna mawasiliano, kila mtu na lwake.
Jambo la msingi kwa wanandoa ni kujadili tofauti zao pindi linapojitokeza jambo linalomkera mmoja wa wanandoa, kwani hakuna jambo linaloweza kujitatua lenyewe bila kutatuliwa na wandoa husika. Kuacha jambo lolote bila kulitafutia suluhu ni sawa na kutega bomu, ambapo siku likilipuka madhara yake ni makubwa sana.
Unaweza kukuta mwanandoa anakereka na mambo madogo madogo ya mwenzi wake lakini hasemi, ingawa yanamkera kupita kiasi akitegemea huyo mwenzi wake atajua na kuacha, thubutu…..inapotokea siku yeye amekosa jambo dogo tu na huyo mwenzi wake akamsema, basi atatumia fursa hiyo kuanza kujibu mapigo kwa kueleza yale yanayomkera kutoka kwa mwenzi wake, na hapo itakuwa kila mtu anavutia kwake kama mwamba ngoma………na aamini nawaambia kuwa kamwe hawezi kupatikana mshindi katika jambo hilo, kwani mjadala huo unaweza kutoka nje ya mada kila mmoja akijitahidi kutafuta makosa ya mwenzi wake hata yale yaliyotokea wakati wa uchumba wenu ili mradi vurugu tupu.
Inatakiwa wanandoa wajadili kila jambo linalojitokeza hadi kulipatia suluhu, vinginevyo ni kuichimbia ndoa yenu kaburi la mapema. Wakati mwingine unaweza kukuta mwanamke analalamika juu ya kutoridhishwa kwake na matumizi ya mumewe, na hapo mume naye ataanza kukumbusha juu ya matumizi yasiyo ya lazima yaliyofanywa na mke huko nyuma. Mke naye hataridhika atakumbushia jambo lingine na lingine hadi hata mada iliyokuwa ikijadiliwa inasahaulika.
Jambo lingine ni kujumuisha mambo, matumizi ya maneno kama, mara nyingi, kila wakati au mara kwa mara si mazuri sana. Unaweza kukuta mtu mwenzi wake amekosea jambo halafu mwenzie anamwambia “Kila mara huwa unafanya hivi” au mara nyingi huwa unafanya hivyo…..Hii ni hatari kwa ustawi wa wanandoa, kwani kwa kujumuisha ni sawa na kumwambia mwenzi wako kuwa kila mara yeye ndiye mkosaji.
Kwa haya niliyoyaeleza hapa sina maana kwamba huu ndio muarobaini pekee wa kuimarisha mahusiano kwa wanandoa, bali ni moja ya mambo muhimu kati ya mengi ambayo yakizingatiwa na wanandoa wote basi ndoa yao itakuwa imara Tujadili pamoja………..

Sunday, May 12, 2013

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE ...BARAKA NA UPENDO VITAWALE KATIKA NYUMBA ZENU

Napenda kuwatakia jumapili njema wote mtakaopita hapa maisha na mafanikio ...naomba wote tusali sala hii...
Salamu Maria, umejaa neema.
Bwana yu nawe
umebarikiwa kuliko wanawake wote,
na Yesu, mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria mtakatifu, Mama wa Mungu,
utuombee sisi wakosefu,
sasa na saa ya kufa kwetu.
Amina.
JUMAPILI NJEMA SANA KWA WOTE....

Saturday, May 11, 2013

PICHA YA WIKI..MAMA NISHUCHE NATAKA KUCHEZA...

Inaonekana mtoto hataki kubebwa au sijui kaona kitu fulani anataka akachukua??? Au wenzangu mwasemaje? ...mmmmhhh nimetamani mchicha na chaina hiyo ngoja nami nianze kulima bustani yangu...JUMAMOSI NJEMA..

Friday, May 10, 2013

UMETOKA MKOA UPI HAPA?

1. Dar es salaam - Utapeli
2. Arusha - Heka heka
3. Mbeya - Matukio
4. Tanga - Majini
5. Dodoma - Ombaomba
6. Mwanza - Fujo
7. Kagera - Misifa
8. Rukwa - Uchawi
9. Kilimanjaro - Ujanja
10. Mara - Ukatili
11. Kigoma - Ubishi
12. mtwara - Umaskini
13. Ruvuma - Ugoni
14. Singida - Upole
15. Tabora – Majungu
16. Shinyanga - Miujiza
17. Morogoro = Starehe

18. Iringa - Ukorofi
19.Zanzibar ???
 20.Pemba ??
NAWATAKIENI MWANZA MWEMA WA MWISHO WA JUMA...

Wednesday, May 8, 2013

UJUMBE WA LEO NI HUU:- MAISHA NI ZAWADI!!

Leo kabla ya kusema neno baya, mfikiria mtu ambaye hawezi kusema.
Kabla ya kulalamika kuhusu ladha ya chakula, fikiria mtu ambaye hana kitu cha kula. Kabla ya kulalamika kuhusu mume wako au mke wako, fikiria mtu ambaye amliliaye Mungu kwa ajili ampe rafiki. Leo kabla ya kulalamika kuhusu maisha. Fikiria mtu ambaye alikwenda mbinguni mapema mno amekufa mapema mno. Kabla ya kunung'unika kuhusu umbali gani unaendesha gari lako, fikiria mtu ambaye anatembea umbali huo kwa miguu yake. Na wakati wewe ni mchovu na ulalamikapo kuhusu kazi yako, fikiria wale wasio na ajira, walemavu, na wale ambao wanataka wangekuwa na kazi kama yako . Na wakati mawazo yanakutawala na kukufanya uwe na huzuni, tabasamu na ufikiri. Wewe ni hai na bado upo.
TUWE NA UHAKIKA NA TUFIKIRI/TUWAZE KWA UHAKIKA!!!! SIKU NJEMA KWA WOTE MTAKAOPITA HAPA.

Monday, May 6, 2013

MTU NA MAZINGIRA...LEO NI USAFI WA NJE....

 Leo tulikuwa katika usafi wa nje..Tulikuwa tumekata miti kama unavyoona hilo lundo hilo. Sheria ni kwamba hakuna kuchoma moto ni lazima kutupa sehemu maalumu...kazi inaendelea.....
 Hapa tumejaza mkokoteni mzima na kufunga kamba kabisa kelekea huko tunakotupa taka----
Na hapa ndiyo sehemu maalumu ya kutupa kwenye haya makontena na halafu mashine yanasaga saga....lakini ni matawi matawi tu.....Hivi ndivyo ilivyoanza JUMATATU YANGU...na sasa ngoja nikapalilie na kutoa majani kwenye maua yangu...Muwe na JUMATATU/MWANZO MWEMA WA JUMA.

Sunday, May 5, 2013

JUMAPILI NJEMA KWA UJUMBE HUU....BABA SHIKAMOO!!!


Ni jumapili ya kwanza ya mwezi huu wa tano..baraka, upendo na amani zitawale katika nyumba zenu. TUPO PAMOJA

Saturday, May 4, 2013

AINA ZA UFUJAJI..HII NI MOJA YA AINA YA UFUJAJI,,UFUJAJI WA KIROHO...

Ni pale ambapo mpenzi anatumia dini au imani ya mwenzake kumwendesha. Kuna wakati anabaini kwamba, kwenye imani ya mpenzi wake kuna kipengele anachoweza kukitumia kumkandamiza mwenzake, ambapo hukitumia.
Kwa mfano, kama imani ya mwenzake inasema mwanamke amtii mumewe, kipengele hicho kitapindwepindwa na mpenzi hadi mfujwaji akubali anayotaka mfujaji, kupitia kipengee hicho.
Lakini pia kumzuia mpenzi kuchiriki kwenye ibada au maombi au huduma yoyote ya imani yake. Kuzuia huku kunaweza kuwa ni kwa moja kwa moja au kwa mbinu za kulaghai na kukashfu. Mara nyingi hata hivyo, kashfa, matusi , kebehi na matumizi ya nguvu hutumika katika sula hili.
Kuna wakati watoto hulazimishwa kufuata imani ambayo mzazi mmoja haitaki na ambayo pengine haikuwa imani ya yeyote kati ya wapenzi wawili. Mpenzi mmoja kabadili  dini wakiwa tayari kwenye ndoa, halafu analazimisha watoto kufuata hiyo dini yake mpya, bila makubaliano na mwenzake ambaye yeye hajabadili dini.
Kuna mkazi mmoja wa Magomeni Mwembechai ambaye aliwahi kuja kwangu, akilalamika kuhusu ndoa yake na mumewe. Alisema, mumewe ameingia kwenye imani mpya. Mume huyo hurejea nyumbani usiku saa tano au sita. anapofika hapo nyumbani huanza kuimba kwa kelele akitukuza imani yake na Mungu.
Mume huyo huwaamsha watoto na kuwataka waimbe usiku huo wa saa tano au sita, akimtaka mke wake naye kujiunga nao. Mke yule aliniambia kwamba, anapojaribu kukataa au kuwatetea watoto kwamba, inabidi walale kwaajili ya kuwahi shule kesho yake, mume huyo humtukana kwa kumwita, ibilisi, mpottevu, mtu wa mataifa, mlaanifu mwenye mapepo wachafu wa ujeuri na kashfa za mataifa, mlaanifu mwenye mapepo wachafu wa ujeuri na kashfa za matusi ya nguoni.
Hii ni aina ya udhalilishaji kupitia dini au imani, ambao ni udhalilishaji wa kiroho. Imani inatumika kutoka maumivu kwa mwingine,
INATOKA KATIKA KITABU CHA MAPENZI KUCHIPUA NA KUNYAUKA....

Friday, May 3, 2013

HUU NI MLO WANGU WA JANA JIONI ..KAZI YA MIKONO YANGU!!!

Hapa chakula ndo kinatoka tu kwenye oven...ni lasagne,,nyama ya kusaga, aina ya pasta, chizi na maziwa..dakika 30 kwenye oven.
 
 
Na hapa ni sahani ya Kapulya ..bila kusahau saladi na kinywaji ni maji

Thursday, May 2, 2013

WANAWAKE NA MIGOROLI ..HAWA NI WAMTINDO/WAREMBO WA WIKI HII...JE UNAWAFAHAMU?

Wanawake/wadada hawa wanaonekana kupenda sana kuvaa mgoroli ..umegundua kitu hapa ni kwamba wote wameachia mkono wa upande mmoja..:-)
Halafu unajua kitu kingine huyo wa juu katabasamu lakini huyu wa chini au mwenye kijani anaonekana yupo mbali kweli kifkra...Unajua ni kitu gani kingine wadada/wanawake hawa wanapenda kufanya?...Karibuni ....

Wednesday, May 1, 2013

SIKUKUU YA WAFANYAKAZI ..MEI MOSI!!!

Mwenzenu nina swali hapa:- Hivi Wafanyakazi ni akina nani? Wakulima akina nani?...Na wafanyabiashara ni nani?.Maana katika akili yangu naona kila kitu ufanyacho na kutoka jasho ni kazi. Naomba tujadili kwa pamoja hapa...JUMATANO YA MEI MOSI IWE NJEMA.....KAPULYA

Tuesday, April 30, 2013

SHUKRANI KWA WOTE MLIOSHIRIKI NASI KATIKA KIPAIMARA CHA BINTI YETU..AMBAYO NI SEHEMU/HATUA YA MAISHA KATIKA MAISHA/KUISHI!!!!

Nachukua nafasi hii na kuwashukuruni wote mliohudhuria siku hii ya kipaimara cha binti yetu iwapo kiukaribu au kwa umbali..Mwenyezi Mungu awazidishie Upendo. Kwa vile Mwanakipaimara anajua kiswahili amesoma maoni ameniagiza kusema AHSANTE SANA kwa kuwa naye kwa siku hii maarufu katika hatua za maisha...AHSANTENI..NA MUWE NA JUMANNE NJEMA..KAPULYA NA FAMILIA.

Sunday, April 28, 2013

JUMAPILI YA LEO NI MAARUFU BINTI YETU CAMILLA ANAPATA KIPAIMARA..HONGERA..

picha ya pamoja baada ya kupata kipaimara Da ´Camilla  hapo katikatika na nywele nyeusi
 
nipo na rafiki
watu walivyofurika

baadhi ya wageni waliokujha kumpongeza Camilla
baadhi ya msosi

 
baada ya misa , sasa hapa nu nyumbani

keki ya karoti
 
kufungua zawadi
Jumapili hii imekuwa ndefu na nyenya baraka nyingi sana katika nyumba yetu ...TUNAMSHUKURU MUNGU KWA SIKU HII...nimeona niwe pamoja nanyi katika siku hii njema, AHSANTE MUNGU....NA HONGERA SANA BINTI CAMILLA

Saturday, April 27, 2013

JUMAMOSI YA LEO TUANGALIE VITENDAWILI VYETU...KITENDAWILI.....

Kwanza nina swali moja hivi kwa nini tunasema KITENDAWILI....na wengine wanajibu...TEGA..???? HAYA KITENDWILI...
1. Huyu mwanamume, huyu mwanamke, hwakutani...
2, Mtoto wangu ninapomtuma mmoja, wanarudi wengi.
3. unga wa kuanika usiku, mchana hakuna.
4. Shamba langu kubwa, ulezi nivunao kiganja kimoja
5. mtu mwenyewe mdogo, watoto wengi.

JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE....NASUBIRI MAJIBU:-)

Thursday, April 25, 2013

TANZANIA INA MAKABILA MENGI NA KILA KABILA LINA MTINDO WAKE WA KUENEZA UTAMADUNI WAKE .HAPA NI NGOMA YA Traditional dance, Kisesa...


Haya jamani ilikuwa zamani kidogo na hizi ngoma zetu za asili..karibuni tucheze...mimi nafikiri ni WASUKUMA HAO ..JE WEWE MWENZANGU UNASEMAJE? MUWE NA WAKATI MMOJA

Wednesday, April 24, 2013

KATIKA MAISHA KUNA KUPENDWA NA KUCHUKIWA NA WATU ....!!! UPENDO!!!

Kupenda/upendo ni kitu cha ajabu sana mara nyingi nimekuwa nimejiuliza kwa nini sisi binadamu tuna upendo tofauti kwa kila mtu. Nikisema hivi nina maana kuna wakati mtu inaweza kutokea unampenda mtu kiasi kwamba huwezi kujizuia. Na cha ajabu mara nyingine uanaweza kumpenda mtu ambaye hujawahi kumwona ana kwa ana(uso kwa uso) na upendo ukawa wa nguvu kali sana.
Halafu sasa inaweza kuwa kinyume kabisa. Yaani watu tunaweza kuwa na chuki. Unaonana na mtu siku moja tu na utasikia simpendi kabisa jamaa huyu. Au hata kuangalia tu picha yake unapatwa na chuki. Nashangaa sana kwa uwezo kama huu ambao MUNGU amatupa na pia SHETANI anaingilia na kuharibu.Swali:- Hivi hii inatokana na nini?
Leo nimeona niimbe mwenyewe ila samahani hamtaisikia sauti yangu:
Upendo, upendo, upendo ni amri ya bwana, Yesu alisema pendaneni, pendaneni kama nilivyowapenda. Nanyi pia, nanyi pia mpendane palipo na upendo Mungu yupo nasi tupendane tupendanex2.
NAWATAKIENI WOTE UPENDO NA AMANI KATIKA KILA MFANYACHO...KAPULYA

 

Tuesday, April 23, 2013

KUNA NJIA NYINGI YA KUITANGAZA BENDERA YETU YA TANZANIA...

Nimependa magauni haya nafikiri safati ijayo nami nitashona maana duh nimepeata hamu kweli--kama tusemavyo ni rangi nzuri na kila moja ina maana yake..tukianzia na..
1. Nyeusi- Huonyesha watu wa Jamuhuri ya Tanzania.
2. Kijani - Huonyesha mimea na ardhi ya Tanzania
3. Njano - Huonyesha utajiri wa mali ya asili.
4. Bluu - Huonyesha bahari inayoziunganisha sehemu za Jamuhuri ya Muungano
Haya ni maelezo  ya Bendera yetu ya Jamuhuri ya Tanzania....Si mnakumbuka tulijifunza darasa la tatu-nne vile au?......Nawatakieni wote JUMANNE NJEMA!!!!

Monday, April 22, 2013

SIMBA WEUPE WA PORI LA LIPARAMBA WILAYANI MBINGA MKOANI RUVUMA....!!!

Juzi nilikuwa naangalia habari ya wanyama pori ambayo ilikuwa kuhusu simba waupe huko Afrika ya kusini,,,Mara nikakumbuka ya kwamba Simba waupe wanapatikana pia katika pori la wanyama la Liparamba wilayani Mbinga mkoani Ruvuma. Ina semekana Wanyama katika pori hii kila mwaka wanahamia kutoka nchini Msumbiji kuingia Tanzania. JE WEWE MWENZANGU UMEWAHI KUONA SIMBA MWEUPE???

Sunday, April 21, 2013

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE WATAOPITA HAPA...MAISHA NA MAFANIKIO

IMANI YA BWANA IWE NANYI...NA UPENDO PIA BARAKA ZITAWALE NYUMBANI MWENU.

Saturday, April 20, 2013

JUMAMOSI ...UJUMBE WANGU NI HUU....

Ukiwa DUNIANI USIHUZUNIKE na usiwe MNYONGE hata kama una UMASKINI kiasi gani. Mungu yuko pamoja nawe na unatakiwa kuzingatia haya:-
1. Usijilaumu kwa lolote lililokutokea
2. Usihofu kuhusu hali uliyo nayo sasa.
3. Usijilinganishe na mtu yeyote duniani.
4. 5. kumbuka Mungu ndie mpangaji wa kila linalokutokea.
6. Usiwaze sana kuhusu kesho waza kuhusu leo.
7. Kukikosa ulichokikusudia yote ni mipango ya Mungu.
MUWE NA SIKU/JUMAMOSI  NJEMA

Thursday, April 18, 2013

KWA MARA NYINGINE TUANGALIE JAMBO HILI :-MTOTO/KIJANA AFUNGA NDOA NA MAMA YAKE MZAZI BAADA YA BABA YAKE KUFARIKI -SONGEA!!!

Katika pitapita nimekutana na hii mimi na Tanzania ...nikakumbuka hii nikaona niweka hapa  maisha na mafanikio... haya hebu wasikilize maelezo yao pia wanajamii wengine...

Sijui hapa itakuwa laani au ni ukosefu wa akili...inasikitisha sana kwa kweli....Jioni njema kwa wote mtakaopita hapa..Bibi kaongea na kingoni bwana :-)

unaikumbuka hii???- KUAMINI KUWA WAMEKAMILIKA NI KUJIDANGANYA BURE!


unaikumbuka hii? ebu soma tena ni vizuri kukumbuka  zilipendwa....karibu

Wiki iliyopita na wiki hii nimekumbuka sana nyumbani, nadhani ni kwa sababu wiki iliyopita tarehe 17 ilikuwa ni tarehe ambao mama yangu alifariki na wiki hii 23/5 imetimia miezi miwili tangu Mdogo wangu alifariki. Kwa kweli nam-miss sana mama yangu pia mdogo wangu.

Nakumbuka ilikuwa kila nikienda likizo, nilikuwa natumia muda mwingi kuwa jikoni na mama yangu nikizungumza naye simulizi za kale za enzi ya utoto wangu.

Ni simulizi ambazo kwa kweli kila nizikumbukapo huwa natamani yale maisha yajirudie kwani kuna mengi ya kufurahisha na ya kuhuzunisha ambayo kwangu mimi nimejifunza mengi kwako.

Lakini lipo jambo moja ambalo nimelikumbuka, ambalo kwa kweli huwa linanifikirisha sana. Jambo lenyewe ni kuhusiana na baadhi ya marafiki zangu kule nyumbani.

Kusema kweli ule ukaribu niliokuwa nao na baadhi ya marafiki zangu umepungua kiasi cha kukatisha tamaa.

Sababu kubwa ni kutokana na kile walichodai kwa nimewatupa kutokana na kutowasaidia kupata wachumba wa Kizungu. Yupo rafiki yangu mmoja mbaye yeye aliwahi kunitamkia wazi kuwa mimi ni mbinafsi kwa kuwa ni mara nyingi ameniomba nimtafutie mchumba wa Kizungu kwa kuwa ninaishi huku ughaibuni lakini nimeshindwa kumtafutia.

Nakumbuka nilimweleza ukweli kuwa siwezi kumsaidia juu ya jambo hilo kwa sababu liko nje ya uwezo wangu, lakini kutokana na labda tuite ufinyu wa kufikiri, nilimpoteza rafiki huyu kwa sababu ya kushindwa kumtafutia mchumba wa kizungu……..yaani kaaaazi kweli kweli.

Hata hivyo nilijiuliza swali moja, kuwa hivi hakuna wanaume huko nyumbani mpaka mtu aamue kutafuta mchumba wa Kizungu? Je ni mapenzi au ni Uzungu unaotafutwa hapo?

Lakini kwa upande mwingine sikumshangaa sana kwa sababu kwa huko nyumbani ipo silka ya baadhi ya watu ambao wanaamini kwamba kuoa au kuolewa na Mzungu ni jambo la kujivunia sana. Huwa nimezoea kauli za baadhi ya watu kule nymbani kila niendapo likizo wakisema, ‘siyo mwenzako yule, kaolewa na Mzungu’ .

Yaani mpaka leo hii bado kuna baadhi ya watu wanaamini kuwa kuoa au kuolewa na mzungu ni jambo la kifahari na la kujivunia. Kinachotafutwa sio mapenzi tena ni huo uzungu..

Kuna baadhi ya watu wamefikia hatua ya kuamini kuwa sisi waafrika ni duni na wenzetu weupe ni bora na waliokamilika.

Lakini nadhani makosa hayo hayakuanza leo, yameanzia mbali sana. Kwani kizazi na kizazi tumekuwa tukiaminishwa kuwa wazungu ni bora zaidi yetu sisi.

Kwa mfano, mtu kufanya mambo yake kwa umakini na anayefuata muda huyo ataitwa ni mzungu, au mtu asiyependa majungu, uzinzi, uasherati na umbeya naye ataitwa kuwa ni mzungu. Nakumbuka wakati nikisoma kule nyumbani, ilikuwa kama kuna mwalimu ambaye ni mwadilifu kwa wanafunzi na anayewajali, utawasikia wanafunzi wakisema, ‘yule mwalimu ni mzungu’

Yaani kipimo cha kufanya mambo kwa uadilifu na kuwajali wengine kimekuwa kikihusishwa na uzungu, mpaka imefikia mahali kila mtu anatamani kuolewa au kuoa mzungu wakiamini kuwa hao wamekamilika.

Hata huko makazini napo watu wanaochapa kazi kwa uadilifu wanafananishwa na wazungu. Wakati mwingine huwa nacheka kwa sababu naamini hao wanaoamini kwamba mtu kuwa mzungu anakuwa amekamilika ni wazi kwamba hawawafahamu watu hao.

Kwamba kuwa mzungu ni kutokuwa na tabia mbaya, kama uvivu, udokozi, kutojali muda, kusengenya, umbeya, wivu, au kijicho, uzinzi, uasherati, ushoga na tabia zote mbaya tunazozijua hapa duniani, nikujidanganya bure.

Nasema kuamini hivyo ni kujidanganya, kwa sababu kwa wale wanaoishi huku ughaibuni au wale wanaofanya kazi na hawa wenzetu huko nyumbani, watakuwa ni mashahidi wangu.

Kama mlikuwa hamjui ni kwamba hawa wenzetu nakubali kuwa wapo waadilifu na wenye tabia nzuri, lakini pia wapo wenye tabia za ajabu kama uvivu, udokozi, kutojali muda, kusengenya, umbeya, wivu, au kijicho, kutojiamini, uzinzi, uasherati, ushoga na tabia zote mbaya tunazozijua hapa duniani.

Ule udhaifu tulio nao pia wenzetu hawa wanao tena wenzetu hawa wamepitiliza. Ila kutokana na kudanganywa na TV na hizo kauli za wazee wetu tumejikuta tukiamini kitu ambacho hakipo.

Mie wakati mwingine huwa nashangaa pale ninapokutana na baaadhi ya Watanzania wenzangu ambao wanaishi au wamewahi kuishi huku ughaibuni wanapozungumza kwa kubana pua kama hawa wenzetu. Wanashindwa kujua kwamba ile ni lafudhi ambayo inatokana na lugha yao. Ni kama pale unapokutana na Mmakonde, Mngoni au Msukuma au Mpare anapoongea Kiswahili kwa lafudhi ya lugha yao.

Mbona wenzetu kwa mfano Wanaijeria au Wakenya wanaongea kwa lafudhi ya lugha zao. Ni rahisi sana kumtambua Mkenya au Mnaijeria kutokana na lafudhi yake pale anapoongea Kiingereza, tofauti na sisi ambapo Tunajitahidi kubana pua mpaka tunajisahau hata pale tunapoongea Kiswahili.
Na ndio maana kuna baadhi ya wanawake huko nyumbani na hata huku ughaibuni wamefikia hatua sasa wanaukataa uafrika na kuanza kujichubua kwa mikorogo ili kuutafuta weupe.

Kuna wakati nilipokuwa huko nyumbani nilishangaa kuwaona baadhi ya wasichana ambao nawajua kabisa rangi zao kuwa ni weusi kama mimi lakini wamekuwa weupe mpaka wanatisha! Tabu yote hiyo ni ya nini?

Tumefikia hatua sasa kila jambo linalofanywa na hawa wezetu tunaiga, na ndio sababu siku hizi tabia kama za ushoga, usagaji na tabia nyingine chafu tunazozishuhudia huku zimetamalaki huko nyumbani.

Sisi kama Watanzania tunazo tabia nzuri ambazo hawa wenzetu wanazitamani sana tofauti na tunavyodhani. Kwa mfano, sisi ni kawaida mtu kuamka na kupita nyumba mbili tatu na kuwajulia majirani zake hali, au kuingia nyumba yoyote na kama akikuta chakula akala bila wasiwasi.

Kwa upande wa Misiba au harusi watu wamekuwa wakichangiana na kusaidiana kwa hali na mali, yaani tumekuwa na ushirikiano wa hali ya juu tofauti na wenzetu hawa.

Kuwa mzungu haimaanishai kuwa mwadilifu wala kuwa na tabia nzuri, bali tabia nzuri inatokana na tabia ya mtu na malezi kwa ujumla wake, hakuna mahusiano yaliyopo kati ya uadilifu, tabia nzuri na uzungu. Nasisitiza kuwa hakuna kitu kama hicho, ni kujidanganya bure.

Inashangaza kuona kwamba, badala ya kujivunia tabia hizi nzuri tulizo nazo ambazo hata hivyo wenzetu wanazitamani, tunatamani za kwao ambazo nyingi ni mbaya na zenye kuumiza.
Tubadilike………………

Wednesday, April 17, 2013

BIBI KIDUDE AMEFARIKI DUNIA MAPEMA ALFAJIRI LEO..UTAKUKUMBUKWA DAIMA!!

Hapa ni Bi Kiduka katika uhai wake akipiga ngoma..
Upumzike kwa amani utakumbukwa daima.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...